“Mlinzi mmoja wa ndani alishtuka aliposikia kishindo cha kitu kudondoka. Aligeuka upesiupesi lakini akaridhika alipokuta ni mwenzake ila akashindwa kuelewa kwa nini mwenzake huyo aanguke. Hata hivyo aliachana na Murphy na kuendelea na lindo lake huku akivuta msokoto mfupi wa bangi. Lakini, yule mlinzi hakutembea hatua nyingi kabla ya kusimama na kujiuliza maswali kichwani. Kwa nini mwenzake huyo atoke nje ambako ndiko alikuwa amepangiwa na ambako ndiko waliambiwa kuwe na ulinzi imara na ndiyo maana wakawekwa saba? Kwa nini aanguke ndani ya ua bila hata ya kumsemesha chochote? Kwa nini hakumpigia redio kwamba alikuwa akiingia ndani ili asiwe na wasiwasi? Alipowaza sana aliamua asiwe na pupa. Aliamua kumfuata mwenzake, aliyekuwa mbele yake, ili amwambie kitu na washirikiane.”
Quote by Enock Maregesi
Book:Kolonia Santita
Work
Kolonia Santita
Browse quotes and source details for this work. more
Author
You May Also Like
“It’s the invention of clothes, not nature, that made “private parts” private.”
“If love wasn't conditional, everybody would be in love with everybody.”
“Man usually sees what he is looking for; seldom what he is looking at.”
“The civilized man is technologically ahead of — intellectually behind — his time.”
“The less knowledgeable a nation is, the more 'miracles' the nation has.”
“We are all 'foreigners' to [the remainder of: the human race minus our countrymen].”