Quotessence
Home / Quotes / Quote by Enock Maregesi

Quote by Enock Maregesi

“Taabini hii ni ngumu sana kwangu kuandika pamoja na kwamba ni miaka mitatu kamili toka giza liingie. Mwaka 2014, Novemba 4, nilimpoteza bibi yangu mpendwa, Martha Maregesi, aliyefariki dunia kutokana na ukongo wa kiharusi, na tutamkumbuka daima. Alikuwa na roho ya kipekee; na kifo chake kiliwagusa wengi, pamoja na kwamba aliishi maisha kamili, zaidi ya siku 25550, siku 5110 zaidi, ambazo ndizo tulizopangiwa na Mungu. Mapenzi ya mtu kwa bibi yake ni mapenzi ya kipekee. Nadhani Mungu aliwapa mabibi wote uwezo maalumu wa kuwapenda wajukuu zao, na kufanya maisha yao yatimie, kuwafanya wawe binadamu wazuri na wenye maadili mema. Alichangia pakubwa katika malezi yangu ya utotoni; na aghalabu naweza kukumbuka nikiwa naye jikoni akipika, huku mimi nikifanya kazi nyingine, lakini wakati huohuo akinifundisha mambo kadha wa kadha ya kunikomaza kimaisha. Bibi hakuwa tu bibi. Alikuwa mlezi, rafiki na mtu aliyenihamasisha sana katika maisha. Kifo kinaleta huzuni lakini kinaleta tumaini. Naamini bibi yangu atakwenda mbinguni, kwa sababu naamini alitubu dhambi zake akisaidiwa na wachungaji. Wachungaji hao walimtembelea kila siku, nyumbani au hospitalini, akiwa kitandani kwake akiugua. Bibi yangu alitimiza wajibu wake. Alizaliwa, aliishi, na alikufa katika toba. Siku nitakapokufa ningependa kuzikwa jirani na alipozikwa bibi yangu, ili Yesu atakaporudi tufufuke pamoja.”

Quote by Enock Maregesi

Author

Enock Maregesi

Browse famous quotes and profile details for Enock Maregesi. more

You May Also Like

“- Ho-ho-ho! a strigat uriașul spre ei în timp ce aproape că și-l dezlipea pe Bibi de pe gheata sub care îl prinsese. Ați fost cuminți, copii, anul ăsta? - Dar tu ai fost? s-a răstit Ada la namila care-i aduna și-i împingea grămadă înspre marginea aleii. - Nu chiar, a râs uriașul cu toată gura lui mare și spărgându-le timpanele, dar judecătoarea mi-a mai dat o șansă, că eram la prima abatere. Ia ziceți, piticilor, dacă fac așa, de cine vă aduc aminte? a întrebat el umflându-și abdomenul, punându-și mâinile pe burtoi și răcnind sălbatic: Ho-ho-ho! Mericrismăs! - Vreau la mami! a anunțat Bibi, în timp ce ceilalți rămăseseră interziși.”

“We are broken. Our ways are apart. Still we laugh together and taunt. We fight and get hurt... Still we don't stop! We spread love among us, With the scent of believe. We write on live. Our dreams are shattered. We think to move on, But scared to miss each other. We smirk when someone scolds, But we drink a jar of poison each time. We die and born everyday. We rely on each other. We get furious. We tease and never step back. We listen but never act on. For public we are mature, But among us we are childish. We act like ninjas among us. And we love to stay like this... Among us forever! Because we are siblings.”