“Kuna vitu vitatu ndani ya mtu: kuna hiari, kuna ufahamu, na kuna mwili. Hiari inatawaliwa na Mungu; ufahamu unatawaliwa na malaika mwema; mwili unatawaliwa na nyota lakini chini ya usimamizi wa malaika wema: malaika wema walisimamisha jua na mwezi kwa ajili ya Yoshua na wana wa Israeli juu ya Gibeoni na katika bonde la Aiyaloni, walirudisha jua nyuma kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda na kwa ajili ya nabii Isaya, na waliifanya dunia ‘kuvaa koti’ ghafla wakati wa kusulubiwa kwa Mwanakondoo wa Mungu Anayeondoa Dhambi. Moyoni ni mahali patakatifu. Hata malaika wema hawawezi kuona ndani ya moyo wa mtu, ni Mungu pekee mwenye uwezo wa kufanya hivyo, na alichokihifadhi Mungu ndani ya moyo huo ni hiari ya mtu ya kuchagua mema au mabaya.” WorldHeartGodBodyStarsSunAwarenessMoonManFree WillThree ThingsMunguSinsDuniaMtuLamb Of GodDhambiMwiliJoshuaJudahIsraelitesJuaYoshuaNyotaGood AngelsMalaika WemaUfahamuMoyoniWana Wa IsraeliGibeonGood AngelHiariHoly PlaceMalaika MwemaMweziGibeoniYudaBonde La AiyaloniKing HezekiahMahali PatakatifuMfalme HezekiaMwanakondoo Wa MunguNabii IsayaProphet IsaiahValley Of AijalonVitu Vitatu Author:Enock Maregesi