“Maisha tunayoishi ni mafupi, maisha ya mbinguni ni ya milele. Fundisha familia yako upendo na hofu ya Mungu, kwani hiyo ndiyo akili kushinda zote. Hekima ya kutunza familia inapatikana katika kitabu cha Mithali cha Agano la Kale.” LoveLifeBrainForeverIntelligenceLife Is ShortOld TestamentMaishaFear Of GodAkiliUpendoMileleHofu Ya MunguAgano La KaleBook Of ProverbsFamily WisdomHeaven S LifeMaisha Ya MbinguniHekima Ya Kutunza FamiliaKitabu Cha MithaliMaisha Ni Mafupi Author:Enock Maregesi
“Usiifundishe familia yako anasa. Ifundishe upendo, unyenyekevu na hofu ya Mungu. Ukiifundisha anasa utahatarisha maisha ya mbinguni ya familia yako, na ya kwako pia.” LoveFamilyLuxuryHumblenessFamiliaFear Of GodUpendoHofu Ya MunguUnyenyekevuAnasaHeaven S LifeMaisha Ya Mbinguni Author:Enock Maregesi
“Mungu hatakubali kuwa na mtu katika ufalme wake ambaye hatakubali kutawaliwa naye. Usikubali kutawaliwa na Ibilisi, kubali kutawaliwa na Mungu. Ni jukumu letu kuanza kuishi sasa kama vile tutakavyoishi mbinguni. Shetani anataka uwe na hekima ya duniani ili akupumbaze. Lakini hofu ya Mungu ndiyo msingi wa hekima ya kweli. Ukitaka asikupumbaze, pokea Roho ya Mungu kwa kubatizwa. Ukiipokea Roho ya Mungu utajua mambo ya Mungu, ambayo dunia haiwezi kujua.” WisdomHeavenKingdomLuciferFear Of GodHekimaMbinguniIbilisiHofu Ya MunguUfalme Author:Enock Maregesi