“Sasa litambua hili: ushindi ni lazima kwa sababu Daudi wetu Yesu Kristo ameshamshinda Goliati wao Shetani. Amemshinda ili aishi ndani yetu na anaishi ndani yetu. Lakini hatutaweza kumshinda Shetani na malaika wake mpaka tutambue kuwa wapo na tuamini kuwa Mungu atawashinda kama tutampa nafasi ya kufanya hivyo kwa kuwa watiifu kwake.” VictoryJesus ChristYesu KristoUshindiNgao Kamili Ya MunguPanopliaDaudi WetuGoliati WaoOur DavidTheir Goliath Author:Enock Maregesi
“Kuwa na huruma kwa malaika anayekulinda ni kujifunika kwa silaha kamili ya Mungu. Ukijifunika kwa panoplia utamrahisishia kazi malaika wako, aliyepewa jukumu na Mwenyezi Mungu kukulinda.” CompassionAngelMalaikaHurumaNgao Kamili Ya MunguPanopliaFull Armor Of GodSilaha Kamili Ya Mungu Author:Enock Maregesi
“Mungu anataka tujifunike kwa ngao yake. Yaani, tuwe na imani iliyokomaa katika Bwana na yeye atatufunika. Maana ya kauli hiyo ni kwamba kila kiungo cha miili yetu kuanzia unyayo hadi kichwa lazima kifunikwe kwa silaha ya Mungu, ambayo Mungu anaiita panoplia. Panoplia haimo katika kamusi ya Kiswahili au Kiingereza, lakini maana yake ni ‘ngao kamili ya Mungu’. Hii si tu silaha ya Mungu. Ni silaha kamili ya Mungu tunayotakiwa kujifunika kwayo.” GodFaithMunguShieldImaniNgao Kamili Ya MunguPanopliaNgaoSilaha Ya MunguWeapon Of God Author:Enock Maregesi