“Watoto hawatakiwi kuchungwa kupita kiasi hasa katika kipindi hiki ambacho dunia imekata tamaa. Ukiwanyima watoto uhuru wa kuwa watoto leo watakuwa na uhuru wa kuwa watoto kesho. Uhuru utakaowanyima wakiwa wadogo watakuja kuutafuta baadaye wakiwa wakubwa. Wakiutafuta baadaye wakiwa wakubwa hawataeleweka vizuri katika jamii. Wape watoto uhuru wanaostahili kupata lakini si uhuru wa kila kitu.” WorldChildrenTodayFreedomSocietyYouthTomorrowProtectionEldersDuniaLeoWatotoUhuruJamiiOverprotectionKeshoUlinziDunia Imekata TamaaWorld Has Given UpWakubwaKuchungwaKuchungwa Kupita KiasiUlinzi Wa Kupita Kiasi Author:Enock Maregesi
“Kumwamini Mwenyezi Mungu wakati wa raha ni rahisi kuliko kumwamini Mwenyezi Mungu wakati wa shida, na utahitaji imani kuendelea kumwamini wakati wa dhiki. Vipindi vigumu katika maisha yetu hutokea kwa kila mmoja wetu. Kuamini ya kwamba Mungu ana makusudi ya lazima kukuondolea vikwazo katika maisha yako ni vigumu sana wakati mwingine, lakini imani ndicho kitu cha muhimu zaidi unachotakiwa kuwa nacho katika kipindi hiki ambacho dunia imekata tamaa. Amani ya Mungu, ambayo huzidi hekima na maarifa yote ya kibinadamu, ni kuliamini neno la Mungu kwamba ni la kweli. Bila imani hutaweza kumfurahisha Mungu. Imani ni ufunguo wa nguvu, uwezo na neema ambavyo Mungu ametupangia. Kwa ufupi, Mungu ni mkubwa kuliko wewe na matatizo yako.” LifeGodFaithAbilityPowerGraceDifficultyObstaclesProblemsComfort ZoneMunguKeyMaishaMatatizoImaniMwenyezi MunguNguvuUwezoGod AlmightyDeliberatelyPeace Of GodDunia Imekata TamaaWorld Has Given UpMakusudiNeemaUfunguoVikwazoAmani Ya MunguDhikiWakati Wa Raha Author:Enock Maregesi
“Dunia imekata tamaa. Matatizo ya watu yamekuwa makubwa kuliko ukombozi wa maisha yao. Sekunde moja ya toba inaweza kukupa ufalme wa mbinguni. Hujachelewa.” PeopleWorldLifeSalvationRepentanceProblemsKingdom Of HeavenDuniaMaishaWatuSecondMatatizoSekundeDunia Imekata TamaaUfalme Wa MbinguniWorld Has Given UpTobaHujachelewaUkomboziYou Are Not Late Author:Enock Maregesi