“Mungu hakutuumba ili tuwe roboti, ambayo hufanya kazi kama ilivyoelekezwa. Alituumba ili tuwe huru. Yaani, tuwe na uwezo wa kuchagua mema au mabaya – ndiyo maana akaweka Mti wa Maarifa ya Mema na Mabaya katika Bustani ya Edeni – ndiyo maana akamtuma Shetani kuwajaribu Adamu na Hawa, wazazi wetu wa kwanza.” GodEvilCapacityGoodParentsSatanFreeMunguGarden Of EdenShetaniRobotUwezoMabayaMemaWazaziHuruBustani Ya EdeniMti Wa Maarifa Ya Mema Na MabayaOur First ParentsWazazi Wetu Wa KwanzaRoboti Author:Enock Maregesi
“Biblia inatuagiza tuwaheshimu wazazi wetu ili siku zetu zipate kuwa nyingi hapa duniani. Mzazi wako akikutuma kuiba mheshimu kwa kukataa.” RespectBibleParentsBibliaHeshimaWazazi Author:Enock Maregesi
“Uwezekano wa watoto wa ukoo mmoja kuoana ni mkubwa kwa sababu damu ina nguvu ya uvutano. Kuhakikisha kwamba familia zinafahamiana na kushirikiana katika mambo mbalimbali ni jukumu la wazazi.” ChildrenResponsibilityBloodParentsFamiliesFamiliaWatotoDamuClanWazaziGravitational ForceUkooJukumuNguvu Ya Uvutano Author:Enock Maregesi
“Asiyefundishwa na wazazi wake atafundishwa na dunia kwa kudharaulika.” ParentsIdiotWazaziAsiyefundishwaAtafundishwa Na DuniaWill Be Taught By The World Author:Enock Maregesi
“Isipite siku hata moja katika maisha yako bila kusema hata kimoyomoyo kwa wazazi wako na kwa watu wote wanaokupenda kwamba unawapenda, kwani siku moja hawatakuwepo tena.” PeopleParentsDayYour LifeWatuMaisha YakoWazaziSiku Author:Enock Maregesi
“Sigara zilizidi kuvutwa, ndani ya nyumba, na magaidi wale wawili, wakati Murphy akisinzia kudanganyia kama kweli nguvu zilishamwisha. Alimfikiria tena mpenzi wake Sophia, safari hii sana. Alimkumbuka Debbie; hakujua alikuwa wapi na hakujua mama yake angefanya nini kama Debbie angekufa, na Murphy ndiye aliyetoka naye. Debbie alimuuma zaidi. Alimkataza kufa kwa ajili ya mchumba wake. Sasa alikufa kwa ajili ya mtu ambaye hakumjua. Murphy alijilaumu kumtongoza na kumchukua kwao na kulala naye na kula chakula chake cha kifalme. Wazazi wake wangejisikiaje kama angekufa, tena katika mazingira ya kutatanisha kama yale. Kufa alijua angekufa; lakini Mungu angemsaidia, awaage watu wake.” GodCriminalsParentsCigaretteMunguWatuJohn MurphyJohn Murphy AmbilikileDebbie Patrocinio AbregoMagaidiSigaraWazaziMazingira Ya KutatanishaMucky CircumstancesMchumba FiancéeSophia Kaswiga Book:Kolonia Santita Source: Kolonia Santita