Quotessence
Home / Topics / Christian Of The Church Quotes

Christian Of The Church Quotes

Browse 3 quotes about Christian Of The Church.

Christian Of The Church Quotes

“Shetani anatisha. Ana macho makubwa manane: macho ya serafi, macho ya mwanadamu, macho ya simba na macho ya tai, na ana mabawa makubwa sita yenye urefu wa futi sita mpaka nane kila moja. Ana rangi ya bluu, bluu iliyoiva, ambayo ni sehemu kubwa ya rangi ya kuzimu, na macho makubwa kama nguva wa Afrika. ‘Mtu’ wa namna hiyo akikwambia njoo nikupige kojoa kwanza ndiyo uende. Kukaa karibu na ‘mtu’ wa namna hiyo ni kujitafutia matatizo makubwa. Kuepukana naye, usiwe mkristo wa Shetani, usiwe mkristo wa kanisa, usiwe mkristo wa dini, kuwa Mkristo wa Yesu Kristo. Kwa maneno mengine, usiwe mkristo wa kufuata bendera, usiwe mkristo wa kinafiki – kuwa Mkristo wa kweli.”

“Unapokuwa mbali na Mungu unakuwa mbali na mwanga, unakuwa gizani, unakuwa mbali na joto, unakuwa katika baridi ya milele. Unapokuwa katika baridi ya milele rangi ya ngozi yako itabadilika na kuwa bluu. Macho yako yatakuwa makubwa kama ya nguva. Bluu maana yake ni kuwa mbali na maarifa ya Mungu. Nguva maana yake ni kuwa mbali na utukufu wa Mungu. Kuwa karibu na maarifa ya Mungu na utukufu wa Mungu, usiwe mkristo wa kanisa, usiwe mkristo wa dini, kuwa Mkristo wa Yesu Kristo.”