Quotessence
Home / Topics / Kitabu Quotes

Kitabu Quotes

Browse 6 quotes about Kitabu.

Kitabu Quotes

“Kitabu cha KOLONIA SANTITA kinaweza kusomwa na watu wenye umri wa kuanzia miaka 13 na kuendelea. Katika umri wa miaka 13 fikra za mtoto huanza kuwa na maono na utambuzi wa vitu mbalimbali. Watoto katika umri huu wanao uwezo wa kuchambua dhana kadha wa kadha za kinadharia, na hali kadhalika wanao uwezo wa kuchambua nadharia tata zisizokuwa na uhakika, kama nadharia ya KOLONIA SANTITA.”

“Kama George Bush angekuwa na amani ndani ya moyo wake na Saddam Hussein angekuwa na amani ndani ya moyo wake Vita ya Ghuba isingetokea. Vilevile, katika kitabu cha ‘Kolonia Santita’, kama Rais wa Tume ya Dunia angekuwa na amani ndani ya moyo wake na kiongozi wa Kolonia Santita angekuwa na amani ndani ya moyo wake Kolonia Santita isingepigana na Umoja wa Mataifa. Taifa lisingepigana na taifa, na mataifa yasingepigana na magaidi.”

“Kama kuna swali maarufu kuliko yote katika kitabu cha 'Kolonia Santita' ni "Кто Вы, где Вы от, и почему Вы в Москве?" lililoulizwa na товарищи (Komredi) Anatoly-Chaika, baada ya kumfikisha Murphy katika 'dacha' ya Kolonia Santita ya Yugo Zapadnaya. Murphy hakumwelewa Chaika. Lakini mwenzake na Chaika (Vladimir) alipouliza kwa tafsiri, "Wewe ni nani, unatoka wapi, na unafanya nini Moscow?" Murphy alimwelewa na kucheka akiwa amenuna. Bila swali hilo asingeokoka.”