“Damu, mto wa maisha unaotiririsha maji yake mwilini kwa kusukumwa na pampu za moyo na kuchujwa na fizi za mapafu, inaundwa na seli na maji yaitwayo utegili au maji ya damu, ambayo kazi yake ni kusafirisha oksijeni na virutubisho katika kila sehemu ya mwili, ndani yake kuna roho. Mungu alitoa kafara ya damu kwa ajili ya Adamu na Hawa katika Bustani ya Edeni. Ibrahimu alitoa kafara ya damu kwa ajili ya Israeli ijapokuwa mapenzi ya Mungu kwa Israeli yalikwisha baada ya kusulubiwa kwa Yesu Kristo. Wana wa Israeli walitoa kafara za damu kwa ajili ya wokovu wa watoto wao wa kwanza na watoto wa kwanza wa wanyama wao nchini Misri. Mungu alitoa kafara ya damu ya Yesu Kristo nchini Israeli kwa ajili ya wanadamu wote duniani. Damu ya mwanakondoo ina nguvu kuliko maombi, imetiwa wakfu na Mwenyezi Mungu na ina uhusiano mkubwa na ulimwengu wa roho. Ukifunikwa na damu ya mwanakondoo Shetani hatakuona. Shetani asipokuona, utafanikiwa.” HumansGodBodySpiritWaterBloodJesus ChristIsraelSatanEgyptOxygenIsraeliAbrahamPrayersAdam And EveMunguGod S WillNutrientsShetaniCellYesu KristoPlasmaMwenyezi MunguMwiliGod AlmightyBlood SacrificeOrdainedRohoWanadamuDamuIsraelitesMaombiMajiRiver Of LifeAdamu Na HawaBlood Of The LambMapenzi Ya MunguIbrahimuBustani Ya EdeniDamu Ya MwanakondooMisriOksijeniSeliWana Wa IsraeliThe Garden Of EdenUlimwengu Wa RohoVirutubishoWakfuCrucifixion Of Jesus ChristKafara Ya DamuSpritual WorldAir SacsAlveoliFizi Za MapafuHeart PumpsKusulubiwa Kwa Yesu KristoMaji Ya DamuMto Wa MaishaPampu Za MoyoUtegili Author:Enock Maregesi
“Mungu ni mtakatifu na kwa maana hiyo hatendi dhambi. Hivyo, hauwi wala hatesi. Tunajiua na kujitesa wenyewe. Ametupa hiari ya kuchagua mema au mabaya. Lakini anamtumia Shetani kama wakala wake wa kutoa adhabu kwa binadamu pale tunapoenenda sawasawa na machukizo yake. Damu ina nguvu kuliko Shetani na ina nguvu kuliko kuzimu. Unapojifunika kwa damu ya Mwanakondoo, Shetani hataweza kukuona. Hivyo, hataweza kukudhuru. Lakini usipojifunika kwa damu ya Mwanakondoo, Shetani atakuona. Hivyo, atakudhuru. Atakudhuru kwa sababu Mungu atakuwa ameruhusu akudhuru, kwa sababu ya uhuru wa kuchagua mema au mabaya aliotupatia, ijapokuwa ana uwezo wa kuzuia asikudhuru. Kwa mtindo huo Mungu anakuwa ametoa adhabu kwa binadamu.” HumansGodFreedomHolyGoodPunishmentSatanChoiceBadMunguSinsShetaniAbhorrenceAgentDhambiBinadamuMabayaMemaUhuruBlood Of The LambAdhabuDamu Ya MwanakondooWakalaHiariMachukizoMtakatifu Author:Enock Maregesi
“Damu ya Mwanakondoo ina nguvu kuliko maombi. Mungu hauwi, Anamtumia Shetani kama wakala wake wa kutoa adhabu kwa binadamu. Ukifunikwa na damu ya Mwanakondoo Shetani, ambaye ni wakala, hatakuona. Lakini Mungu atakuona. Bila kafara ya damu hakuna msamaha wa dhambi. Bila kafara ya damu hakuna mafanikio.” HumansGodSuccessSatanPrayersMunguShetaniForgiveness Of SinsAgentMafanikioBinadamuBlood SacrificeMaombiBlood Of The LambDamu Ya MwanakondooWakalaKafara Ya DamuMsamaha Wa Dhambi Author:Enock Maregesi
“Hutaweza kumiliki watu bila damu ya Mwanakondoo.” PeopleWatuBlood Of The LambDamu Ya Mwanakondoo Author:Enock Maregesi