“Wanasayansi wanaamini kuwa Yesu atarudi tarehe 29 Julai 2016. Tarehe hiyo kitu kikubwa sana kitatokea katika dunia yetu kitakachosababisha tetemeko kubwa la ardhi, litakalosababishwa na kubadilika kwa ncha za dunia, tendo litakalosababisha mionzi ya gama kutoka kwenye jua ifike duniani na kuua kila kitu kinachoonekana katika uso wa dunia hii. Watakatifu watafufuka na kumlaki Kristo mawinguni, ambaye anakuja kuwachukua wateule na kumweka Shetani kifungoni kwa miaka 1000. Hayo yote, wanasema, yatatokea ndani ya siku 11 kuanzia leo. Yaani, kusini mwa dunia kutakuwa kaskazini mwa dunia, kaskazini mwa dunia kutakuwa kusini mwa dunia. Kitendo hicho kitafanya dunia ikose kinga ya sumaku iitwayo ‘magnetosphere’ ambayo hukinga dunia dhidi ya mionzi ya gama kutoka kwenye jua. Mionzi hiyo hugonga ukuta wa ‘magnetosphere’ kila baada ya dakika 8 kwa mwendokasi wa kilometa milioni 1080 kwa saa; na kusambazwa katika ncha za dunia ambapo aghalabu huchanganyikana na oksijeni na kutengeneza kitu kinaitwa ‘aurora’, au mwanga wa ncha, ambacho ni maajabu mengine ya angani. Mwaka 2012 wanasayansi walisema ncha za dunia zingebadilika lakini hazikubadilika. Je, muda umefika sasa wa kuwaamini wanasayansi? Biblia ni chuo cha Mungu. Soma Biblia kupata maarifa.” WorldJesusChristKnowledgeSunBibleSatanOxygenScientistsSaintsDuniaShetaniWondersAurora2012BibliaEarthquakeYesuMaarifaJuaKristoWanasayansiOksijeni1000 YearsMaajabuMiaka 1000WatakatifuElectsMwaka 2012Wateule1080 Million Kilometers Per Hour29th July 20168 MinutesChuo Cha MunguDakika 8Gamma Rays RadiationsGod S CollegeKaskazini Mwa DuniaKilometa Milioni 1080 Kwa SaaKinga Ya SumakuKusini Mwa DuniaMagnetosphereMionzi Ya GamaMwanga Wa NchaNcha Za DuniaNorthern WorldSouthern WorldTarehe 29 Julai 2016Tetemeko La ArdhiWorld Poles Author:Enock Maregesi
“Damu, mto wa maisha unaotiririsha maji yake mwilini kwa kusukumwa na pampu za moyo na kuchujwa na fizi za mapafu, inaundwa na seli na maji yaitwayo utegili au maji ya damu, ambayo kazi yake ni kusafirisha oksijeni na virutubisho katika kila sehemu ya mwili, ndani yake kuna roho. Mungu alitoa kafara ya damu kwa ajili ya Adamu na Hawa katika Bustani ya Edeni. Ibrahimu alitoa kafara ya damu kwa ajili ya Israeli ijapokuwa mapenzi ya Mungu kwa Israeli yalikwisha baada ya kusulubiwa kwa Yesu Kristo. Wana wa Israeli walitoa kafara za damu kwa ajili ya wokovu wa watoto wao wa kwanza na watoto wa kwanza wa wanyama wao nchini Misri. Mungu alitoa kafara ya damu ya Yesu Kristo nchini Israeli kwa ajili ya wanadamu wote duniani. Damu ya mwanakondoo ina nguvu kuliko maombi, imetiwa wakfu na Mwenyezi Mungu na ina uhusiano mkubwa na ulimwengu wa roho. Ukifunikwa na damu ya mwanakondoo Shetani hatakuona. Shetani asipokuona, utafanikiwa.” HumansGodBodySpiritWaterBloodJesus ChristIsraelSatanEgyptOxygenIsraeliAbrahamPrayersAdam And EveMunguGod S WillNutrientsShetaniCellYesu KristoPlasmaMwenyezi MunguMwiliGod AlmightyBlood SacrificeOrdainedRohoWanadamuDamuIsraelitesMaombiMajiRiver Of LifeAdamu Na HawaBlood Of The LambMapenzi Ya MunguIbrahimuBustani Ya EdeniDamu Ya MwanakondooMisriOksijeniSeliWana Wa IsraeliThe Garden Of EdenUlimwengu Wa RohoVirutubishoWakfuCrucifixion Of Jesus ChristKafara Ya DamuSpritual WorldAir SacsAlveoliFizi Za MapafuHeart PumpsKusulubiwa Kwa Yesu KristoMaji Ya DamuMto Wa MaishaPampu Za MoyoUtegili Author:Enock Maregesi
“Potassium Cyanide si hatari inapokuwa nje. Ni hatari inapojichanganya na asidi za tumboni ambapo hubadilika na kuwa gesi ya 'hydrogen cyanide'. Gesi ya 'hydrogen cyanide' ni miongoni mwa sumu hatari zaidi ulimwenguni. Mtu akimeza kidonge cha 'cyanide' atapata madhara makubwa. Kichwa chake kitamuuma hapohapo na atachanganyikiwa akili. Ngozi yake itakuwa nyekundu, kwa sababu damu yake itakuwa nyekundu zaidi – kutokana na kuzidi kwa oksijeni katika damu. Mwili hautakuwa na uwezo tena wa kuchukua oksijeni kutoka katika damu ili uitumie, kwa hiyo damu itazidi kuwa na oksijeni zaidi. Atapumua kwa shida. Mapafu yake yatafanya kazi vizuri lakini mwili wake hautakuwa na uwezo wa kutumia oksijeni yoyote – hivyo atadhani ana matatizo katika mfumo wake wa kupumua. Atazimia. Yaani, oksijeni haitafika kwenye ubongo. Atapata kifafa na atatapika nyongo. Ubongo wake utashindwa kufanya kazi na atakuwa mahututi ndani ya sekunde kumi! Baada ya hapo moyo wake utasimama kufanya kazi, na atafariki dunia.” WorldMindHeartBodyUniverseBrainBloodDangerSeriousRedBreathingDamagePoisonGasStomachSecondsOxygenLungsAcidHeadacheSkinHeadHydrogenDuniaEpilepsyMoyoAkiliUlimwenguCyanideMwiliPotassiumDamuUbongoMadharaPillSekundeHatariMapafuOksijeniSumuGesiTumboKichwaAsidiHydrogen CyanideKichwa KuumaKidongeKifafaKupumuaMahututiNgoziNyekunduPotassium Cyanide Author:Enock Maregesi
“Mafanikio unapaswa kuyataka kama unavyotaka hewa. Hewa ni kitu cha muhimu zaidi kuliko kitu kingine chochote kile ulimwenguni. Ukipewa hewa au shilingi bilioni kumi chagua hewa.” SuccessAirOxygenMafanikioHewaUlimwenguniOksijeniIn The UniverseShilingi Bilioni KumiTen Billion Shillings Author:Enock Maregesi