“Msamaha ni uamuzi wa makusudi wa kuachilia hisia za chuki au kisasi juu ya mtu au kikundi cha watu ambaye amekuumiza au ambacho kimekuumiza, bila kujali kama anastahili au kinastahili msamaha wako. Wataalamu wanaosoma au kufundisha msamaha huweka bayana ya kuwa, unaposamehe, hutakiwi kusitiri au kukana uzito wa kosa ulilofanyiwa. Msamaha haumaanishi kusahau wala haumaanishi kupuuza, au kujisingizia, makosa ambayo mtu amekufanyia au kikundi cha watu kimekufanyia. Ijapokuwa msamaha unaweza kusaidia kujenga uhusiano ulioharibika, haukulazimishi kupatana na mtu aliyekukosea au kumfanya asiwajibike kisheria kwa makosa aliyokufanyia. Badala yake, msamaha humletea yule anayesamehe amani ya moyo; na humpa uhuru kutokana na hasira aliyokuwa nayo, juu ya yule aliyemkosea.” FreedomForgivenessAngerHarmonyRevengeExpertsPersonLegalMtuMsamahaHasiraUhuruMakosaOffencesWataalamuKisasiAmani Ya MoyoDeliberate DecisionMaulamaaThey DeserveTo ForgetA Group Of PeopleAnastahiliFeelings Of HatredHisia Za ChukiHutakiwi KusitiriIt DeservesKikundi Cha WatuKinastahiliKisheriaKujenga Uhusiano UlioharibikaKujisingiziaKukana Uzito Wa KosaKupatanaKupuuzaKusahauPeace Of The HeartTo Build A Broken RelationshipTo IgnoreTo Slander OneselfUamuzi Wa MakusudiUnaposameheWhen You ForgiveYou Should Not Camouflage Author:Enock Maregesi
“Mungu akikubariki kipaji chako watu watasema ni laana. Maisha yako ni sawa na mto. Unakoelekea ni baharini. Lakini sasa umefika kwenye mlango wa bahari. Unahangaika upite wapi kufika baharini, ambapo utaogelea kwa kadiri utakavyoweza. Utakapofika baharini, watu, badala ya kusema umebarikiwa, watasema umelaaniwa, badala ya kukuita malaika, watakuita shetani. Mafanikio hayapimwi kwa pesa au mali kiasi gani unayo, mafanikio yanapimwa kwa amani ya moyo au maisha ya watu kiasi gani umeboresha.” PeopleLifeGodSuccessMoneySeaTalentOceanAngelPropertyCurseSatanRiverMunguShetaniMaishaWatuPeace Of HeartMaliPesaMafanikioLaanaKipajiMalaikaAmani Ya MoyoMtoBahariniEntrance To The SeaMlango Wa Bahari Author:Enock Maregesi