“Mbegu tunazopanda leo ni mazao ya msimu ujao. Ukipanda mbegu mbaya utavuna mabaya. Ukipanda mbegu nzuri utavuna mazuri. Ukitenda mabaya leo kesho yako itakuwa mbaya. Ukitenda mazuri leo kesho yako itakuwa nzuri. Okoa kesho leo kwa kupanda mbegu nzuri na kuzimwagilia kwa imani na upendo kwa watu. Mungu ataleta mvua, jua na ustawi wa mazao yako. Panda mbegu ya msamaha kwa maadui zako, uvumilivu kwa wapinzani wako, tabasamu kwa marafiki zako, mfano bora kwa watoto wako, uchapakazi kwa kazi zako, uadilifu kwa waajiri wako na kwa wafanyakazi wako pia kama unao, ndoto kwa malengo yako, na uaminifu kwa marafiki zako wa ukweli. Kila mbegu irutubishwe kwa mapenzi huru yasiyokuwa na masharti yoyote, au mapenzi huru yasiyokuwa na unafiki wa aina yoyote ile. Usifiche vipaji vyako. Ukiwa kimya utasahaulika. Usipopiga hatua utarudi nyuma. Usiwe na hasira, wivu au ubinafsi.” PeopleLoveChildrenGodTodayFaithEvilSunDreamsHonestyFriendsTomorrowIntegrityForgivenessRainAngerPerseveranceSmileSeedsGoalsGoodSelfishnessEmployersEnemiesCropsTalentsMunguEmployeesIndustriousSeasonRole ModelWatuLeoImaniWatotoUpendoMsamahaMaaduiMabayaHasiraJuaOpposersMarafikiNdotoMbeguUbinafsiVipajiKeshoUaminifuUvumilivuGood SeedsMalengoMazuriUchapakaziTabasamuUadilifuWaajiriBad SeedsMazaoMbegu MbayaMbegu NzuriMfano BoraMsimuMvuaWafanyakaziWapinzani Author:Enock Maregesi
“Toa msamaha usiokuwa na masharti yoyote kwa yeyote aliyekukosea kwa sababu, dhambi iliyofanya mkosane ilitoka kwa Shetani. Kwa mfano, usiseme umesamehe lakini hutasahau, sema umesamehe na umesahau.” SinConditionsForgivenessSatanShetaniDhambiMsamahaMasharti Author:Enock Maregesi
“Msamaha si jambo dogo. Watu wadogo, watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri, hawawezi kupambana na changamoto za msamaha. Msamaha ni kwa ajili ya watu wenye macho kama ya tai wanaoweza kuona mbali ambao wako tayari kushindwa vita ili washinde vita. Hewa inaingia ndani ya mapafu na kutoka; chakula kinaingia ndani ya mwili na kutoka; mwanamasumbwi anapigana bila kugombana; injini ya gari haiwezi kusukuma gari mbele au nyuma bila kutoa hewa katika paipu ya ekzosi. Lakini kile kinachoingia moyoni mwako hakitoki! Maumivu yanapoingia ndani ya moyo yanapaswa kutoka nje kama yalivyoingia kwa sababu, yasipotoka yatatengeneza sumu ndani ya moyo wako na yatatengeneza sumu ndani ya roho yako pia. Sumu hiyo itahatarisha safari yako ya mbinguni na Mungu hatakusamehe tena. Badala ya yule aliyekukosea kuumia, utaumia wewe uliyekosewa. Yesu anaposema samehe saba mara sabini hatanii. Usiposamehe, hutasamehewa.” HeartWarSoulGodBodyPainJesusAirCarFoodForgivenessSevenPoisonLungsVitaMunguYesuEngineBoxerMwiliMsamahaRohoSabaExhaustHewaSmall PeopleChakulaGariSeventyMapafuMoyoniSumuMaumivuInjiniChallenges Of ForgivenessChangamoto Za MsamahaEagle Like EyesLimited CapacityMacho Kama Ya TaiMwanamasumbwiPaipu Ya EkzosiSabiniSafari Yako Ya MbinguniUwezo MdogoWatu WadogoYour Journey To Heaven Author:Enock Maregesi
“Msamaha ni uamuzi wa makusudi wa kuachilia hisia za chuki au kisasi juu ya mtu au kikundi cha watu ambaye amekuumiza au ambacho kimekuumiza, bila kujali kama anastahili au kinastahili msamaha wako. Wataalamu wanaosoma au kufundisha msamaha huweka bayana ya kuwa, unaposamehe, hutakiwi kusitiri au kukana uzito wa kosa ulilofanyiwa. Msamaha haumaanishi kusahau wala haumaanishi kupuuza, au kujisingizia, makosa ambayo mtu amekufanyia au kikundi cha watu kimekufanyia. Ijapokuwa msamaha unaweza kusaidia kujenga uhusiano ulioharibika, haukulazimishi kupatana na mtu aliyekukosea au kumfanya asiwajibike kisheria kwa makosa aliyokufanyia. Badala yake, msamaha humletea yule anayesamehe amani ya moyo; na humpa uhuru kutokana na hasira aliyokuwa nayo, juu ya yule aliyemkosea.” FreedomForgivenessAngerHarmonyRevengeExpertsPersonLegalMtuMsamahaHasiraUhuruMakosaOffencesWataalamuKisasiAmani Ya MoyoDeliberate DecisionMaulamaaThey DeserveTo ForgetA Group Of PeopleAnastahiliFeelings Of HatredHisia Za ChukiHutakiwi KusitiriIt DeservesKikundi Cha WatuKinastahiliKisheriaKujenga Uhusiano UlioharibikaKujisingiziaKukana Uzito Wa KosaKupatanaKupuuzaKusahauPeace Of The HeartTo Build A Broken RelationshipTo IgnoreTo Slander OneselfUamuzi Wa MakusudiUnaposameheWhen You ForgiveYou Should Not Camouflage Author:Enock Maregesi
“Upendeleo na msamaha ni sumu na baraka ya usuluhishi miongoni mwa watu kwa mpangilio huo. Yaani, upendeleo ni sumu ya usuluhishi, msamaha ni baraka ya usuluhishi. Usuluhishi wenye msamaha, usiokuwa na upendeleo wowote, ni dawa ya uhusiano mwema miongoni mwa watu. Upendeleo ni sumu ya usuluhishi – Msamaha ni kiuasumu cha usuluhishi.” PeopleRelationshipBlessingForgivenessPoisonReconciliationAntidoteFavorWatuMsamahaBarakaSumuUhusianoUpendeleoKiuasumuRespectivelyUsuluhishiKwa Mpangilio Huo Author:Enock Maregesi
“Kama umefanya au umesema kitu kibaya na ukasema ukweli mbele ya mtu au ya watu, omba msamaha kupata tena kibali cha umma.” PeopleTruthForgivenessApprovalPersonPublicThingWatuMtuUkweliMsamahaKituKibaliUmma Author:Enock Maregesi
“Wataalamu wanaosoma au kufundisha msamaha huweka wazi kwamba unapomsamehe mtu, huwezi kupotezea au kukana uzito wa kosa alilokufanyia. Kusamehe ni hali fulani inayotoka ndani ya moyo wa mtu, ikiwa na hali ya uhuru wa hiari wa mtu mwenyewe kuamua kuachilia kile kinachomuumiza, pasipo kuwepo masharti ya aina yoyote ile kwa mtu aliyemuumiza.” HeartFreedomClearConditionsForgivenessExpertsPersonFreedom Of ChoiceMtuMoyoMsamahaUhuruMashartiWataalamuTo ForgiveKusameheMaulamaaUhuru Wa HiariUnapomsamehe MtuWaziWhen You Forgive Someone Author:Enock Maregesi
“Msamaha si jambo rahisi. Tunapoumizwa, au watu wetu wa karibu wanapoumizwa, tendo la kusamehe linaweza kuwa gumu kuliko matendo yote. Lakini, tambua kwamba msamaha ni mchakato wa muda mrefu unaohitaji ujasiri mkubwa kuuanza hadi kuukamilisha, ongea na watu wanaoelewa maana ya msamaha ili wakuongoze katika mchakato huo. Vilevile, tambua kwamba hata wewe umewahi kufanya makosa na unahitaji msamaha, tambua kwamba suluhisho kamili linahitaji matendo kutoka kwa aliyekosea na kwa aliyekosewa. Wengine hupendwa kwa sababu wanastahili, lakini wengine wanastahili kwa sababu hupendwa. Mungu anatupenda kwa jinsi tulivyo hata kama tunajiona hatustahili. Hivyo, jithamini.” CourageForgivenessGod Loves UsValue YourselfMsamahaUjasiriTalk To PeopleIt S Not EasySi Jambo RahisiThey DeserveA Long Time ProcessAliyekoseaAliyekosewaAll ActsJinsi TulivyoJithaminiMatendo YoteMchakato Wa Muda MrefuMungu AnatupendaOngea Na WatuOthers Are LovedPerfect SolutionSuluhisho KamiliTendo La KusameheThe Act Of ForgivingThe OffendedThe OffenderThe Way We AreTunapoumizwaWanastahiliWengine HupendwaWhen We Are Hurt Author:Enock Maregesi
“Msamaha si kwa ajili ya watu wenye mabawa ya kuku, ni kwa ajili ya watu wenye macho ya tai. Kua kuujua msamaha.” PeopleForgivenessWatuGrow UpChicken WingsMsamahaEagle EyesMacho Ya TaiKuaMabawa Ya Kuku Author:Enock Maregesi
“Mtu akikuomba msamaha msamehe. Usipomsamehe hutasamehewa na aliyetusamehe.” ForgivenessManMtuMsamaha Author:Enock Maregesi
“Mbegu ni neno la Mungu. Mfano bora, msamaha, ndoto, tabasamu, uadilifu, uaminifu, uchapakazi na uvumilivu ni maneno ya Mungu. Kwa hiyo mfano bora, msamaha, ndoto, tabasamu, uadilifu, uaminifu, uchapakazi na uvumilivu ni mbegu. Watu ni ardhi. Panda mbegu ya mfano bora kwa watoto wako, msamaha kwa maadui zako, ndoto kwa malengo yako, tabasamu kwa marafiki zako, uadilifu kwa waajiri wako na kwa wafanyakazi wako pia kama unao, uaminifu kwa marafiki zako wa ukweli, uchapakazi kwa kazi zako na uvumilivu kwa wapinzani wako. Kila mbegu irutubishwe kwa imani na upendo kwa watu.” ChildrenForgivenessSeedsWord Of GodEnemiesWatotoMsamahaMaaduiMbeguNeon La Mungu Author:Enock Maregesi
“Mbegu ni neno la Mungu. Mfano bora, msamaha, ndoto, tabasamu, uadilifu, uaminifu, uchapakazi na uvumilivu ni maneno ya Mungu. Kwa hiyo mfano bora, msamaha, ndoto, tabasamu, uadilifu, uaminifu, uchapakazi na uvumilivu ni mbegu. Watu ni ardhi. Panda mbegu ya mfano bora kwa watoto wako, msamaha kwa maadui zako, ndoto kwa malengo yako, tabasamu kwa marafiki zako, uadilifu kwa waajiri wako na kwa wafanyakazi wako pia kama unao, uaminifu kwa marafiki zako wa ukweli, uchapakazi kwa kazi zako na uvumilivu kwa wapinzani wako. Kila mbegu irutubishwe kwa imani na upendo kwa watu. Katika mfano huu ukuaji unawakilisha utakaso, ambao ni muundo wa taswira ya Mungu ndani yetu kwa kuishi kama anavyoishi yeye kwa nguvu ya Roho Mtakatifu. Tunachotakiwa kufanya baada ya kupanda mbegu ni kutimiza wokovu wetu sisi wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka. Kutimiza wokovu wetu sisi wenyewe ni sawa na mvua, jua, palizi, mbolea, ili mavuno yaweze kuwa ya uhakika.” ForgivenessSalvationSeedsHoly SpiritEnemiesMsamahaMaaduiRoho MtakatifuMbeguWokovu Author:Enock Maregesi
“Yesu alipokuwa msalabani watu wengi walimzunguka. Askari wa Kirumi aliyekuwa na chongo, na mkuki, alikuwa na jukumu la kumtesa Yesu hadi kufa kwa amri ya Pilato. Yesu alipolia kwa sauti kuu, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?”, yule askari alikurupuka na kumwendea Yesu. Lakini Yesu alishakata roho. Kuthibitisha kama Yesu alishakata roho, askari alimchoma Yesu mkuki kwenye mbavu kwa nguvu zake zote. Mkuki huo ukamtoboa Yesu hadi upande wa pili, ukatoboa hata moyo wake. Askari alipochomoa mkuki, damu na maji viliruka na kupiga jicho lake bovu. Papo hapo askari akapona na kuona vizuri. Alipoona kweli amepona na kuona vizuri, askari alipiga kelele, alipiga magoti na kuomba Mungu amsamehe dhambi zake. Msamaha una nguvu kuliko dhambi. Askari huyo atakwenda mbinguni. Haijalishi umechukia watu kiasi gani. Haijalishi umetesa watu kiasi gani. Haijalishi umeua watu kiasi gani. Haijalishi umetenda dhambi kiasi gani. Mungu anachotaka kutoka kwako, tubu.” HeartGodEyeJesusHeavenForgivenessApologyRepentRibsCrossMunguSinsYesuDhambiMoyoMsamahaMbinguniMany PeopleSpearBlood And WaterMkukiDamu Na MajiMsalabaniAskari Wa KirumiRoman SoldierEloi Eloi Lama SabakthaniJichoWatu WengiAmri Ya PiratoChongoMbavuMono EyedPirate OrdersTubu Author:Enock Maregesi