“Maskini na tajiri wana mawazo tofauti. Maskini hudhani utajiri ni chanzo cha matatizo. Tajiri hudhani umaskini ni chanzo cha matatizo. Maskini hudhani ubinafsi ni kitu kibaya. Tajiri hudhani ubinafsi ni kitu kizuri. Maskini ana mawazo ya kupata pesa bila kufanya kazi. Tajiri ana mawazo ya kupata pesa kwa kufanya kazi. Maskini hudhani tajiri ana tabia ya kuringa. Tajiri hupenda kuzungukwa na watu sahihi wenye mawazo sawa na ya kwake. Maskini hutengeneza pesa kwa kufanya kazi asizozipenda. Tajiri hutengeneza pesa kwa kufanya kazi anazozipenda. Maskini hudhani kuwa tajiri lazima usome sana. Tajiri hudhani kuwa tajiri si lazima usome sana. Maskini hutamani mambo mazuri ya wakati uliyopita. Tajiri hutamani mambo mazuri ya wakati unaokuja. Maskini huamini ili uwe tajiri lazima ufanye kitu fulani. Tajiri huamini ili uwe tajiri lazima uwe kitu fulani. Maskini hupenda kuburudishwa kuliko kuelimishwa. Tajiri hupenda kuelimishwa kuliko kuburudishwa. Maskini ana woga. Tajiri hana woga. Maskini hufundisha watoto wake jinsi ya kupambana na maisha. Tajiri hufundisha watoto wake jinsi ya kuwa matajiri. Maskini hana nidhamu ya mapato na matumizi. Tajiri ana nidhamu ya mapato na matumizi. Maskini hufanya kazi kwa bidii kupata pesa. Tajiri hutumia pesa kupata pesa. Maskini ni mdogo kuliko matatizo yake. Tajiri ni mkubwa kuliko matatizo yake. Maskini huamini unahitaji pesa kupata pesa. Tajiri huamini utapata pesa kwa kutumia pesa za wengine. Maskini ana wivu wa chuki. Tajiri ana wivu wa maendeleo. Fikiri kama anavyofikiri tajiri. Ukifikiri tofauti na anavyofikiri tajiri, utakufa maskini.” LifeChildrenPastFearWealthPoorMoneyPovertyRichFutureThoughtsSelfishnessThinkRich PeopleOthersSomethingSmallBrandBigMaishaMaskiniPesaTajiriRight PeopleWatotoUtajiriWengineExpenditureMawazoWogaRevenuesUbinafsiUmaskiniMapatoFikiriMatajiriMdogoWatu SahihiMatumiziMkubwaJealous Of DevelopmentJealous Of HateKitu FulaniKuburudishwaKuelimishwaTo Be EducatedTo Be EntertainedWakati UliyopitaWakati UnaokujaWivu Wa ChukiWivu Wa MaendeleoChanzo Cha MatatizoSource Of Problems Author:Enock Maregesi
“Mawazo ya kukata tamaa yanaweza kusababisha tukamtengeneza au kumbuni tena Mungu kwa mfano wetu sisi wenyewe, mfano ambao kwa kawaida ni tofauti kabisa na mfano unaozungumzwa ndani ya Biblia. Hivyo tunaishia kutumikia mfano badala ya kumtumikia Mungu wa kweli.” IdeasGodDespairBibleImageMunguTrue GodBibliaMawazoKukata TamaaMfanoOur ImageMfano WetuMungu Wa Kweli Author:Enock Maregesi
“Siri ya utajiri ni mawazo ya mtu. Maisha unayoishi uliyataka mwenyewe. Amka uishi. Hii ndiyo siri kubwa ya utajiri kuliko zote ulimwenguni. Ukifikiria chanya maisha yako yatakuwa chanya, ukifikiria hasi maisha yako yatakuwa hasi. Unachofikiria ndicho unachokuwa. Siri ya mafanikio yako ni jumla ya mambo unayoyawaza.” LifeIdeasPositiveNegativeWake UpMaishaMawazoAmkaChanyaHasiThe Secret Of SuccessSecrets Of WealthSiri Ya MafanikioSiri Ya Utajiri Author:Enock Maregesi
“Kila mtu ana tabia, matendo, mawazo na akili yake tofauti na mtu mwingine hapa duniani. Usimdharau mtu ukidhani ana akili kama za kwako au anafikiri kama unavyofikiri wewe kwani kila mtu aliumbwa kivyake na Mwenyezi Mungu. Unaweza kudhani unamjua mtu kumbe humjui. Heshimu kila mtu kama unavyojiheshimu kwa sababu, kila mtu ni wa pekee. Kama tunavyotofautiana katika vidole na macho ndivyo tunavyotofautiana katika tabia, matendo, mawazo, imani, maadili na akili. Usimdharau mtu usiyemjua au unayedhani unamjua.” MindIdeasFaithAttitudeUniqueFingersManMoralsEyesMachoMtuImaniAkiliMwenyezi MunguActsGod AlmightyMawazoTabiaMaadiliMatendoPekeeVidole Author:Enock Maregesi
“Kinachotokea katika dunia hii si kitu kizuri cha kuzoea au hata kufikiria. Hivyo tuna haki ya kuwa na mawazo, hasira na wanyonge kuhusiana na suala zima la maisha yetu hapa duniani. Hata hivyo hali hii itabaki kuwa hivyo kwa sababu Mungu ametaka iwe hivyo kwa sasa. Kwa maana hiyo, hekima ni kukubaliana na mapenzi ya Mungu. Lazima tukubaliane na kisichoweza kufikirika kuweza kubadilika.” WorldLifeThoughtsAngerDuniaMaishaWill Of GodHasiraMawazoMapenzi Ya Mungu Author:Enock Maregesi
“Ukiwaza kitu kwa dakika moja na sekunde nane – huu ni utafiti wangu tu – hicho kitu kitaanza kujiumba kwa ajili yako sehemu fulani ulimwenguni. Ukiamini kwa kiasi cha kutosha kwamba umekipata, utakipata. Haijalishi kama una elimu au huna. Hiyo ndiyo siri kubwa zaidi ya utajiri kuliko zote duniani – MAWAZO YAKO.” UniverseWealthSecretEducationThoughtsResearchSiriUlimwenguUtajiriElimuMawazoUtafiti1 Minute 8 SecondsDakika 1 Na Sekunde 8 Author:Enock Maregesi
“Siri kubwa ya utajiri kuliko zote duniani ni mawazo yako.” WealthSecretThoughtsSiriUtajiriMawazo Author:Enock Maregesi
“Kabla hujaanza … pangilia mawazo.” BeforeMawazoArrangeInner DialoguesKablaMazungumzo Ya NdaniPangilia Author:Enock Maregesi
“Kabla hujaanza kufanya chochote, au kusema chochote, pangilia mawazo.” DoSayBeforeAnyMawazoArrangeFanyaSemaInner DialoguesKablaMazungumzo Ya NdaniPangiliaChochote Author:Enock Maregesi
“Maskini ana mawazo ya kupata pesa bila kufanya kazi. Tajiri ana mawazo ya kupata pesa kwa kufanya kazi.” PoorMoneyRichThoughtsJobMaskiniPesaTajiriKaziMawazo Author:Enock Maregesi
“Maskini hudhani tajiri ana tabia ya kuringa. Tajiri hupenda kuzungukwa na watu sahihi wenye mawazo sawa na ya kwake.” PoorRichThoughtsBoastingMaskiniTajiriRight PeopleMawazoWatu SahihiTabia Ya Kuringa Author:Enock Maregesi
“Kutokana na utafiti wa kisayansi wa kionairolojia ambayo ni sayansi ya ndoto; wakati tumelala, sehemu yetu ya akili isiyotambua huamka na kuanza kazi; kwa kupangilia mawazo, kuanzia mawazo ya siku iliyopita, na kuimarisha mahusiano baina ya mawazo hayo na matukio ya wakati ujao, huku ikiondoa mawazo yasiyokuwa na maana, kunusuru ubongo usielemewe na msongo. Kazi hiyo hutambuliwa haraka na akili inayotambua, kwa njia ya alamu, lakini akili inayotambua inapagawa kwa sababu haijui akili isiyotambua inamaanisha nini kutuma alamu kama hizo. Kwa hiyo inajaribu kwa kadiri inavyoweza kutunga hadithi kuhusiana na vitu mbalimbali, ambayo baadaye hutafsiriwa kama ndoto. Hii ndiyo sababu tunaota ndoto za ajabu ambazo aghalabu hazina maana yoyote, na hazina maana yoyote kwa sababu hazitakiwi kuwa na maana yoyote, na hazina ujumbe wowote halisi kutoka akilini mwetu. Hayo ni matokeo ya akili kujaribu kusanisi sauti, kutoka katika akili isiyotambua.” IdeasDreamRelationshipsWorkBrainStorySignalsSubconscious MindScientific ResearchConscious MindFuture EventsKaziMawazoNdotoUbongoHadithiAlamuAkili IsiyotambuaAkili InayotambuaKusanisi SautiMahusianoMatukio Ya Wakati UjaoSayansi Ya NdotoScience Of DreamsSynthesiseUtafiti Wa KisayansiWakati TumelalaWhile We Are Asleep Author:Enock Maregesi
“Mwambie mtoto wako maneno mazuri anapokuwa ananyonya na kukuangalia machoni kwa kukukodolea. Maneno utakayomwambia ndiyo yatakayokuwa msingi wa mawazo yake, na ndiyo yatakayoumba maisha yake atakapokuwa mkubwa.” LifeIdeasWordsChildGood WordsMaishaMawazoMtotoManenoManeno Mazuri Author:Enock Maregesi