Quotessence
Home / Topics / Paulo Quotes

Paulo Quotes

Browse 14 quotes about Paulo.

Paulo Quotes

“Kabla ya uasi, Mungu alimpa Shetani na wasaidizi wake ambao ni mapepo mamlaka makubwa juu ya kila kitu hapa duniani; kuanzia angahewa la dunia hadi ardhi ya dunia nzima nasi wakazi wake tukijumuishwa. Abadani tusisahau kwamba, kwa kiasi kikubwa, kupambana kwetu kama Paulo anavyosema ni dhidi ya hawa mapepo na mfalme wao ambaye ni Shetani. Tunaishi katika eneo ambapo hata wao wanaishi. Hawa mapepo wabaya huwatumia maadui wa msalaba wa Yesu Kristo kutekeleza mipango yao kwa lengo la kuwaangamiza marafiki wote wa msalaba wa Yesu Kristo, wanashawishiwa kwa kiasi kikubwa na hizo mamlaka za kimapepo, na kwa sababu wamedanganywa, hawajui hata kidogo kama Shetani anawatumia! Inawezekana hawajatwaliwa na mapepo lakini wanashawishiwa na mapepo kutenda kinyume na mapenzi ya Mungu kwa wanadamu wote.”

“Jambo ambalo Mungu anataka tulitambue ni kwamba hatuko wenyewe katika bahari hii ya hewa. Hata nyangumi na wazira waovu wanapozunguka huko na huko baharini, ambao pia ni mapepo, wanaochukuliwa kama viumbe wabaya na wachafu na wala mizoga, wanaishi katika bahari hii ya hewa pamoja na sisi. Ni muhimu, kwa ajili ya ustawi wetu wa kiroho, kusikia onyo la Paulo katika Waefeso 6:10-12 kwamba vita yetu si dhidi ya hawa viumbe, na wanapambana usiku na mchana kutetea kile ambacho wanaamini ni cha kwao kwa sababu ya haki ya kuwepo hapa kwanza kabla yetu. Dunia, Biblia inatwambia, ilikuwa makazi yao ya kwanza (Yuda 1:6, KJV). Wanatuchukia kwa sababu taratibu tunakuwa Baba na Mwana, na kwa sababu wanajua hii dunia, urithi wetu, itachukuliwa kutoka mikononi mwao na kukabidhiwa kwa wale ambao ni watoto wa Mungu, wale ambao ni marafiki wa msalaba wa Yesu Kristo.”

“O que interessa é que Jesus teve um corpo de verdade. Para tornar-Se realmente humano, Ele teve de nascer, como escreve o apóstolo Paulo em Gálatas 4, de uma mulher e não somente através de uma mulher. Deus não usou Maria como uma "barriga de aluguel", mas usou o seu DNA. A expressão teológica usada para isto é "encarnação", e o princípio por trás é: o que Deus Se torna Deus redime. Deus tornou-Se o que somos — com um corpo de verdade — para que pudéssemos nos tornar filhos Dele. É por isso que o corpo terreno e verdadeiro de Jesus é importante para a nossa fé.”

“Sabato ilianzishwa na Mungu siku ya saba ya uumbaji wake. Siku ya Sabato ni siku takatifu, iliyoko katika Amri Kumi za Mungu, ambayo hatuna budi kuitunza na kuiheshimu. Sheria ya Siku ya Sabato haikufa baada ya kifo cha Yesu Kristo msalabani kama Wakolosai wanavyodai. Wakolosai walifuata falsafa za kipagani, na walizileta falsafa hizo ndani ya mwili wa Kristo ambalo ni kanisa. ‘Usiiamini’ Wakolosai 2:17. Iamini Wakolosai 2:20-23, ambapo Paulo anafundisha Mataifa jinsi ya kuitunza Sabato, na 1 Wakorintho 12:27 ambayo inatoa maana halisi ya Wakolosai 2:17. ‘Mwili wako ni wa Kristo’ ni tofauti na ‘mwili wa Kristo’ na ni tofauti na kanisa. Ukiamini kama mwili wako ni wa Kristo na ni kanisa, utaitunza Sabato.”

“No, I do not believe in fate, that some spirits of the heavens weave the laws of the world to make it so. That is dogma for the foolish, for the universe is quite able to deal with such matters herself, to use her natural laws to guide matter and the spirits. Even so, souls within the world can act to naturally shift the cause of events. Magister Brennark did say that ‘Nothing happens unless we make it so.’ I believe you have made it so, Wolfdon, and how foolish it would be for us to ignore an opportunity that you yourself established, whether you knew you were doing so or not.”

“Hakuna mahali popote katika Agano Jipya ambapo sheria ya Sabato imekomeshwa (Kutoka 31:12-17), kwani Mungu alianzisha Sabato kwa ajili ya wanadamu wote (Marko 2:27). Kinyume cha hapo, Yesu aliitunza (Luka 4:16), Paulo aliitunza (Matendo 17:2) na Wamataifa waliitunza pia (Matendo 13:42-44; 16:13)! Mwandishi wa Waebrania anaandika bila kificho, “Basi, imesalia raha ya Sabato kwa watu wa Mungu” (Waebrania 4:9).”