“Natafuta mwanamke mwenye utu, wema, uaminifu na tabia njema – sifa ambazo ataendelea kuwa nazo hata uzeeni. Sifa hizi zinaweza kubadilika kwa sababu ya maisha au kwa sababu ya mapenzi ya Mungu, lakini mabadiliko haya hayatakuwepo kwa haraka. Sura haidumu. Tabia hudumu.” LifeHumanityHonestyGoodnessBehaviorOld AgeReputationWomanChangesFaceMaishaGood BehaviorWill Of GodMwanamkeTabiaSifaUtuMabadilikoSuraWemaMapenzi Ya MunguUaminifuTabia NjemaBehavior LastsFace Doesn T LastSura HaidumuTabia HudumuUzeeni Author:Enock Maregesi
“Hasanati ni matendo mema. Mema yanatoka kwa Mungu. Mabaya yanatoka kwa Shetani. Mke mwema anatoka kwa Mungu. Mke mbaya anatoka kwa Shetani. Mke mwema ana hekima na busara, ana maadili na tabia njema, ana utu na uchapakazi, ana wema na upendo, na ana aibu kwa wanaume.” MenLoveGodWisdomHumanityEvilGoodnessEthicsShameGoodSatanGood DeedsPrudenceMunguGood WifeShetaniGood BehaviorHekimaUpendoMabayaMemaIndustriousnessUtuWemaAibuMaadiliUchapakaziBusaraHasanatiWanaumeMatendo MemaTabia NjemaBad WifeMke MbayaMke Mwema Author:Enock Maregesi
“Hakuna mtu mwenye akili timamu anayetaka mabaya katika maisha yake. Mwanamume atake mwanamke mwenye matendo mema. Mwanamke atake mwanamume mwenye matendo mema. Misingi ya hasanati ni misingi ya utu. Tukiishi katika misingi ya utu, misingi ya matendo mema, tutaishi sawasawa na mapenzi ya Mungu. Kila mtu anapaswa kuishi na mke au mume aliye mwema.” LifeHumanityEvilWifeHusbandManWomanSaneGood DeedsPersonMaishaMtuWill Of GodFoundationsMwanamkeMabayaMwanamumeUtuMapenzi Ya MunguMkeHasanatiMatendo MemaMisingiMumeAkili Timamu Author:Enock Maregesi
“Unapokutana na mtu, kisha mtu huyo haoneshi dalili yoyote ya kutaka kusalimiwa; je, anataka umsalimie au usimsalimie? Ndugu yangu, onesha lugha ya mwili kuonesha utu.” HumanityRespectRespecting OthersBody LanguageRespecting YourselfHeshimaUtuLugha Ya MwiliJiheshimu Author:Enock Maregesi
“Kuna nguzo saba ambazo hazina budi kuzingatiwa kama unataka kuheshimiwa na kuwaheshimu wengine. Kwanza kabisa jitambue: wewe ni nani na unafanya nini hapa duniani. Halafu, kabla ya kusema jambo lolote kwa mtu yoyote fikiria kwanza maana au madhara ya hilo unalotaka kulisema. Kisha jifunze tamaduni mbalimbali na watendee wengine kama vile unavyotaka kutendewa au kama vile wanavyotaka kutendewa. Jifunze kusamehe na kusuluhisha migogoro katika jamii unamoishi huku ukidumisha heshima na utu kwa binadamu wenzako. Jijengee imani kwa watu, punguza upendeleo, fanya kazi kama timu kwani hakuna ‘mimi’ katika umoja ila kuna ‘sisi’, na jitahidi kwa kadiri ya uwezo wako WOTE kwa manufaa ya wote. Kuwa kiongozi katika kila jambo unalofanya na katika kila kitu unachofanya. Jitahidi kufanya jambo au kitu kwa usahihi kwa kadiri utakavyoweza.” FaithHumanityLeaderTeamSocietyHumanRespectUnityKnow YourselfAccuracyIWeAllConflictsCulturesMimiImaniBinadamuHeshimaSisiKiongoziJamiiFavouritismUtuUmojaWoteMigogoroTimuUpendeleoJitambueKuheshimiwaTamaduniTo Be RespectedUsahihi Author:Enock Maregesi
“Maskini hajali wewe ni nani. Anajali utu ndani ya moyo wako.” HumanityPoorYouWhoMaskiniMoyoWeweUtuNani Author:Enock Maregesi
“Uko wapi ubinadamu wa watu?” PeopleHumanityPeaceCrueltyVitaWarsWatuAmaniUtuUbinadamuUnyama Author:Enock Maregesi