“Mungu alikupa vipaji ili uwanufaishe wengine na si kujinufaisha mwenyewe, na aliwapa wengine vipaji ili kukunufaisha wewe na si kujinufaisha wenyewe, kwa lengo la kuleta mabadiliko chanya katika dunia yetu.” WorldGodPurposePositiveYouYourselfTalentsChangesOthersMunguDuniaWengineWeweVipajiMabadilikoLengoChanyaMwenyewe Author:Enock Maregesi
“Kwa nini watu wana kawaida ya kuona thamani ya mtu baada ya mtu kufariki? Kwa nini watu wana kawaida ya kuona thamani ya pumzi katika kipindi ambacho mtu hana uwezo tena wa kuvuta hewa? Nini thamani ya pumzi? Thamani ya pumzi ni kukufanya uwe wewe na si udongo.” PeopleEarthValueManBreathingYouBreathWhyWatuMtuWeweThamaniUdongoKwa NiniPumziKuvuta Hewa Author:Enock Maregesi
“Mtu akikushauri kufanya kitu ambacho ni kinyume na takdiri ('destiny') ya maisha yako, hata kama huyo mtu hana nia mbaya na wewe, sema 'hapana' kwa hiyo 'ndiyo' yake.” LifeDestinyAdviceManYouYour LifeMaishaMtuSay NoWeweMaisha YakoTakdiriSema HapanaUshauriBad IntentionNia MbayaHer YesHis YesNdiyo Yake Author:Enock Maregesi
“Ukifanya maamuzi kubaliana na matatizo yake yote. Fanya kile ulichosema utafanya, hata kama sehemu ya kile ulichosema utafanya uliinukuu kutoka kwa wengine, hata kama watu hawatakubaliana na wewe.” DecisionsYouProblemsOthersDoMatatizoWengineWeweMaamuziFanyaAgreedKubaliana Author:Enock Maregesi
“Ukiua mtu bila kumwambia kwa nini unamuua anaweza kujua umemuua kwa kumwonea. Akijua umemuua kwa kumwonea roho yake inaweza kukusumbua wewe na familia yako maisha yenu yote. Makachero wa EAC wana leseni ya kuua. Lakini si kuua ovyo kama James Bond. Kila wanayemuua lazima waandike ripoti kwa nini wamemuua. Kachero wa EAC akiua mtu, kwa makosa, kwa bahati mbaya, atalindwa na Mwenyezi Mungu. Atalindwa na Tambiko la Tume ya Dunia.” LifeSpiritMistakeFamilyYouPersonBad LuckFamiliaMaishaMtuReportMwenyezi MunguJames BondGod AlmightyRohoWeweMakosaSpecial AgentLicenceEacBahati MbayaKacheroSpecial AgentsLeseniMakacheroRipotiTambiko La Tume Ya DuniaWodec S Ritual Author:Enock Maregesi
“Maskini hajali wewe ni nani. Anajali utu ndani ya moyo wako.” HumanityPoorYouWhoMaskiniMoyoWeweUtuNani Author:Enock Maregesi
“Hufanani na yoyote katika dunia hii. Unafanana na wewe mwenyewe. Usimdharau mtu, humjui!” WorldAnimalManYouScornDuniaMtuAnyWeweDharauMnyamaWewe MwenyeweYou AloneYoyote Author:Enock Maregesi
“Mimi na wewe na vitu vyote ulimwenguni ni wazito kwa sababu ya 'Higgs Boson', inayojulikana pia kama 'The God’s Particle'. Wanasayansi wa CERN wamekuwa wakiitafuta 'higgs' (iliyojificha ndani ya 'higgs field') kwa zaidi ya miaka hamsini sasa, kwa bajeti ya pauni za Uingereza bilioni sita. Chembe ya 'higgs' ikipatikana itawajulisha wanasayansi jinsi ulimwengu unavyofanya kazi na jinsi ulivyoumbwa, na jibu la kitendawili cha 'Standard Model' litapatikana.” UniverseYouRiddleIAnswerScientistsMimiWeweCernHiggs BosonWanasayansiStandard ModelUlimwenguniJibuKitendawiliHiggsFifty YearsHiggs FieldMiaka HamsiniPauni Bilioni SitaSix Billion PoundsThe God S Particle Author:Enock Maregesi
“Wewe na rais wa nchi: Wewe unajua mambo ya mtaa. Rais wa nchi anajua mambo ya nchi. Anayejua mambo usiyoyajua ni wa kuogopa kama ukoma.” YouWeweRais Wa NchiYou KnowLocal MattersAnayejua Mambo UsiyoyajuaCountry MattersFear As LeprosyKuogopa Kama UkomaMambo Ya MtaaMambo Ya NchiThe President Of The CountryWewe UnajuaWho Knows What You Do Not Know Author:Enock Maregesi
“Ukila kiapo fanya kile ulichoahidi katika kiapo, si kinyume chake hata kidogo, hata kama dunia haitakubaliana na wewe.” WorldYouOathDoDuniaWeweFanyaKiapo Author:Enock Maregesi
“Watu wote ni wa Mungu, watu ni matatizo. Wewe huna mtu, lakini bado unapambana na Mungu kuhusu watu.” PeopleGodManYouProblemsMunguWatuMtuMatatizoWewe Author:Enock Maregesi
“Unapofikia hatua ya kuwa na kila kitu katika maisha, unapokuwa umefanya kila kitu ulichotamani kufanya katika maisha, unakuwa na bahari nzima ndani ya tone ambalo ni wewe. Unaridhika. Wewe si tone tena ndani ya bahari, wewe ni bahari ndani ya tone. Kinachobaki baada ya hapo ni kusaidia jamii iliyosaidia kukulea ulipokuwa mdogo, kuacha alama katika dunia kabla na baada ya wewe kuondoka, bila kujali watu watasema nini juu ya maisha yako.” PeopleWorldSocietyOceanToneYouDuniaWatuDropWeweJamiiBahariBahari Ndani Ya ToneEverything In LifeKila Kitu Katika Maisha Author:Enock Maregesi