Filter quotes by topic
Famous Enock Maregesi Quotes
“Nimewapa watoto wangu kila kitu katika maisha isipokuwa umaskini. Lakini bado wamenishinda.”
“Maskini mwenye pesa nyingi ni tajiri bahili. Tajiri mwenye mifuko iliyotoboka ni tajiri badhiri.”
“Mtu anayesema pesa haijampa furaha hana nia ya kusaidia watu.”
“Toa msaada katika jamii iliyosaidia kukulea ulipokuwa mdogo.”
“Wanaume hujiua kwa sababu ya fedha. Wanawake hujiua kwa sababu ya mapenzi.”
“Shetani akikupa hela chukua. Hiyo hela ameiiba kutoka kwa Baba. Ukishaichukua, toa zaka.”
“Maskini hufanya kazi kwa bidii kupata pesa. Tajiri hutumia pesa kupata pesa.”
“Mungu hataki tuwe maskini, kwani fedha na dhahabu ni mali yake. Anachotaka kutoka kwetu, zaka.”
“Mungu hagawi pesa kwa watu kama watu wanavyofikiria. Anagawa upendo na hekima.”
“Kumbuka kwamba watu wanaokupa pesa bila masharti yoyote wanajisikia vizuri sana kufanya hivyo.”
“Pesa inayokuinua juu ndiyo itakayokushusha chini, kwani hakuna kilevi hapa duniani kama pesa.”