Filter quotes by topic
Famous Enock Maregesi Quotes
“Luka 22:20 ni mwisho wa agano la kale la damu za wanyama na mwanzo wa agano jipya la damu ya Yesu.”
“Ubatizo ni hatua ya kwanza ya wokovu, na Wakristo ni matunda ya kwanza ya Mungu.”
“Usisubiri Mungu afanye kitu ambacho Mungu anasubiri ufanye.”
“Kuna maisha baada ya saa tisa na nusu. Kuwa makini na raia.”
“Mungu hagawi pesa kwa watu kama watu wanavyofikiria. Anagawa upendo na hekima.”
“Kumbuka kwamba watu wanaokupa pesa bila masharti yoyote wanajisikia vizuri sana kufanya hivyo.”
“Pesa inayokuinua juu ndiyo itakayokushusha chini, kwani hakuna kilevi hapa duniani kama pesa.”
“Watu wakiwa wamekasirika ongea nao jibu; usiongee nao tatizo.”
“Sala ni ombi la jambo ambalo si la kawaida. Kufanikisha jambo ambalo si la kawaida lazima utulie.”
“Ukiwa mwaminifu katika mambo madogo utakuwa mwaminifu katika mambo makubwa.”
“Mtu akisema neno usimfuatilie yeye, bali fuatilia neno alilolisema.”
“Jifunze kutoka kwa mwalimu, jifunze zaidi kutoka kwa wenzako.”
“Sheria wakati mwingine inaweza kuonea mtu. Pigana hata tone la mwisho kutetea haki yako.”
“Ubinadamu una kila kitu isipokuwa upendo miongoni mwa watu.”
“Wasifu wa viongozi wa Kolonia Santita ni siri kwa sababu siri ni siri ya mafanikio.”
“Mshukuru sana mtu anayekuchukia, kwani chuki yake hukufanya mpiganaji.”