Quotessence
Home / Authors / Enock Maregesi

Enock Maregesi Quotes

Author

Filter quotes by topic

Famous Enock Maregesi Quotes

“Ndani ya gruneti kuna vitu kumi vyenye uwezo na visivyokuwa na uwezo wa kulipuka kama vile pini, mtaimbo, springi ya mtaimbo, tundu la kuingizia baruti, baruti, fataki, fyuzi, utambi, wenzo na ganda la chuma la pingili kama vipande vya risasi. Pini inapochomolewa, na bomu kurushwa kuelekea kwenye shabaha au kuelekea sehemu nyingine yoyote, wenzo wa usalama huchomoka pia na kuachana na bomu moja kwa moja. Wenzo wa usalama unapochomoka huruhusu mtaimbo ugonge fataki ya kuwashia fyuzi kwa nguvu na kasi kubwa. Fyuzi itawaka kwa sekunde nne kabla ya kuwasha utambi, ambao utawasha baruti ndani ya sekunde moja, kabla ya baruti kulipuka – na kusambaza vipande vya bomu katika kila sehemu ya shabaha.”

“Kuna tetesi kuwa Julius Nyerere alipewa tuzo ya MBE na malkia wa Uingereza akiwa rais wa Tanzania! Lakini aliikataa! Kwa nini? Kwa sababu angeonekana Mwingereza zaidi kuliko Mtanzania! Januari 26, 1996 akapewa Tuzo ya Kimataifa ya Amani ya Mahatma Gandhi ya mwaka 1995, ya kwanza kabisa, iliyotolewa na Serikali ya India. Lakini hiyo pia akaikataa! Kwa sababu Mahatma Gandhi alimwaga damu katika harakati zake za kuwang'oa wakoloni barani Afrika! Kama ni kweli, hakuna kujitolea kuliko huko.”

“Oavsett hur begåvad eller kunnig du är, du kommer aldrig att nå din fulla potential utan sakkunnig vägledning.”

“Det bästa priset livet har att erbjuda är inte en chans att arbeta hårt och vara något i samhället. Det är parfymen Guds som finns inom dig.”

“Beroendet är inte om att använda droger. Det handlar om vad läkemedlet gör att ditt liv.”

“Wakiwa na suti nzito za kijani na madoa meusi (‘Ghillie Suits’) kwa ajili ya kupigania porini; Vijana wa Tume walikuwa na kofia za chuma, miwani ya kuonea usiku (iliyokuwa na uwezo wa kubinuka chini na juu), redio na mitambo ya mawasiliano migongoni mwao juu ya vizibao vya kuzuia risasi, vitibegi vya msalaba mwekundu (‘Blowout Kits’ – katika mapaja ya miguu yao ya kulia, ndani yake kukiwa na pisto na madawa ya huduma ya kwanza), vitibegi vya kujiokolea (‘Evasion Kits’ – katika mapaja ya miguu yao ya kushoto, ndani yake kukiwa na visu na pesa na ramani ya Meksiko) na bunduki za masafa marefu. Kadhalika, Vijana wa Tume waliamua kuchukua Punisher – waliyoafikiana baadaye kuwa ilikuwa nzuri kuliko RPG-7, ‘Rocket Propelling Gun’, ambayo Mogens alipendekeza waitumie kubomolea Kiwanda cha Dongyang Pharmaceuticals; kwa sababu hakutaka kuleta madhara kwa watu waliokuwa hawana hatia.”

“Wakati Ford Bronco inatoka katika Kiwanda cha Dongyang Pharmaceuticals S.A de C.V. (kilichomilikiwa na mkurugenzi mkuu wa 'methamphetamine' wa Kolonia Santita mfanyabiashara wa Kichina kutoka Chaling, katika jimbo la Hunan, kusini ya kati ya China, Li Dongyang; na mkurugenzi wa usalama wa Kolonia Santita kutoka Lomas de Chapultepec, Mexico City, Gortari Manuel) Daniel Yehuda na Radia Hosni, waliokuwa wakipiga picha kila kitu kilichokuwa kikiingia na kutoka kiwandani kwa ajili ya ripoti ya upelelezi wao ya baadaye, waliiona. Lakini, hawakujua kama ilikuwa ikienda Varsovia kumuua Murphy na Sajini Mogens. Bronco ilipofika Varsovia ilisimama kwa fujo mbele ya SUV ya msafara wa Mtoto wa Rais Debbie Patrocinio Abrego, aliyekuwa ndani ya Mgahawa wa Angus akicheza muziki wa 'mariachi' na John Murphy, huku Mogens akilinda usalama wa kamanda wake na usalama wa baa nzima. Kabla majambazi wa Kolonia Santita hawajaleta madhara au fujo yoyote kwa Vijana wa Tume, polisi walifika eneo lile haraka ilivyowezekana! Kwa msaada wa walinzi wa Debbie! Wale majambazi walipekuliwa na kukutwa na bastola moja ya Akdal Ghost, bunduki mbili za AK-47, na picha nne za Vijana wa Tume ndani ya gari yao. Polisi waliwakamata na kuwapeleka katika kituo cha polisi cha Tume ya Dunia kilichopo Zona Rosa, Mexico City.”

“Ili kupambana na matumizi mabaya ya madawa ya kulevya katika jamii ya Tanzania, ni muhimu kutoa elimu kwa Watanzania juu ya madhara yanayoambatana na matumizi ya madawa hayo. Tusipambane na madawa ya kulevya peke yake. Tupambane na elimu ya madawa ya kulevya pia.”

“Kama kuna swali maarufu kuliko yote katika kitabu cha 'Kolonia Santita' ni "Кто Вы, где Вы от, и почему Вы в Москве?" lililoulizwa na товарищи (Komredi) Anatoly-Chaika, baada ya kumfikisha Murphy katika 'dacha' ya Kolonia Santita ya Yugo Zapadnaya. Murphy hakumwelewa Chaika. Lakini mwenzake na Chaika (Vladimir) alipouliza kwa tafsiri, "Wewe ni nani, unatoka wapi, na unafanya nini Moscow?" Murphy alimwelewa na kucheka akiwa amenuna. Bila swali hilo asingeokoka.”

“Murphy alichanganyikiwa. Hakujua nini kilitokea na kwa nini. Ila, ghafla, alipotupa macho kushoto aliona kitu. Joka kubwa lilitambaa, ingawa kwa shida, kwa sababu ya sakafu, na kumfuata kummaliza. Murphy alijua joka hata angefanya vipi, hakuwa na uwezo wa kujikinga. Alipotaka kupiga kelele ili walinzi wa nje waje, Murphy alishindwa. Nyuma ya joka – katika mkia – kuna kitu kiling’aa, kikamshangaza! Muujiza ulimtokea Murphy lakini kitu kikamwambia aite walinzi wa nje ili waje wamuue yule nyoka. Lakini kabla hajapiga kelele, alisikia sauti; si ya mwanamume. Ya mwanamke!”

“Kwa nini mtoto mchanga anapokuwa ananyonya ziwa la mama yake, mara nyingi humwangalia mama yake machoni? Kwa sababu, licha ya macho kuonekana kitu cha ajabu kwake, mtoto mchanga, bila kujitambua, hutamani sana mama yake amwambie neno zuri atakalolitumia baadaye katika maisha yake atakapokuwa mkubwa. Maneno huumba. Ukimwambia mwanao kuwa anaonekana atakuwa jambazi, anaweza kuwa jambazi kweli atakapokuwa mkubwa; ukimwambia kuwa anaonekana atakuwa mwanasheria, anaweza kuwa mwanasheria kweli atakapokuwa mkubwa.”

“Kamera ina athari kubwa sana katika maisha yetu. Inaweza kuharibu taswira ya mtu mbele ya jamii, na inaweza kuharibu maisha ya mtu hali kadhalika. Wasanii wakubwa duniani hawatoki ndani bila ya kuwa nadhifu au bila ya kujipodoa. Kwa nini? Kwa sababu ya wasanii wao wa vipodozi. Wasanii wao wa vipodozi hawataki waajiri wao wawe na taswira mbaya mbele ya wateja wao ambayo ni jamii. Kuwa na taswira mbaya mbele ya jamii kunaweza kusababisha wao (wasanii wa vipodozi) pamoja na waajiri wao, wasiishi vizuri hapa duniani kama wanavyotaka. Kioo ni kitu au mtu. Kama huna uwezo wa kumiliki vipodozi, miliki kioo. Kama huna uwezo wa kumiliki kioo, miliki rafiki. Kioo (hasa kitu) hakina unafiki. Usitoke ndani bila kuridhika na taswira yako.”